Posts

Showing posts from August, 2025

Rozari Takatifu (Matendo ya Mwanga) - Alhamisi

1. Ubatizo wa Yesu Mtoni Yordani Wakati huo Yesu akaja kutoka Galilaya mpaka Yordani kwa Yohana ili abatizwe. Naye Yesu alipokwisha kubatizwa mara akapanda kutoka majini; na tazama, mbingu zikamfunukia, akamwona Roho wa Mungu akishuka kama hua, akija juu yake. Na tazama, sauti kutoka Mbinguni ikisema, "Huyu ni mwanangu, mpendwa wangu, ninayependezwa naye." (Mathayo 3:13, 16-17) Ee Mungu, kwa fadhili zako, kwa maji na Roho Mtakatifu, tunazaliwa katika maisha ya uzima wa milele. Tunakusihi kwa wema wako uendelee kuzimimina baraka zako juu yetu; na kutufanya kuwa wana waaminifu wa taifa lako takatifu. Amina. 2. Yesu Ageuza Maji Kuwa Divai Huko Kana Na siku ya tatu palikuwa na harusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwapo. Yesu naye alikuwa arusini pamoja na wanafunzi wake. Hata divai ilipowatindikia, mamaye Yesu akamwambia, "Hawana divai." Naye mkuu wa meza alipoyaonja yale maji yaliyopata kuwa divai, alimwita bwana harusi, akamwambia, kila mtu kwanz...

Rozari Takatifu (Matendo ya Furaha) - Jumatatu na Jumamosi

1. Malaika Anampasha Habari Maria Kwamba Atakuwa Mama wa Mkombozi Malaika   akamwambia, "Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema; na jina lake utamwita Yesu... Mariamu akasema, "Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema." Ee Bwana, tujalie imani ukubali mapenzi yako daima bila kusitasita. Tunawaombea pia wale wote ambao hawakujui, lakini wanakutafuta kwa moyo mnyofu. 2. Bikira Maria Anakwenda Kumtembelea Elisabeti Basi Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda, akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti. Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu. (Luka 1:39-41) Ee Bwana, ijaze mioyo yetu furaha na shukrani kwa kuwa umetuita kuwa watoto wako. Kwa njia ya pekee tunawaombea wakatekumeni na wale wote ambao kwa mafundisho yao, wanawaongoza kwako. 3. Yesu Anazaliwa Bethlehemu Ikawa, katika kukaa huko, ...

Rozari Takatifu (Matendo ya Uchungu) - Jumanne na Ijumaa

1. Yesu Anatoka Jasho la Damu Akasema, "Aba, Baba, yote yawezekana kwako; uniondolee kikombe hiki; walakini, si kama nitakavyo mimi, bali utakavyo wewe." (Marko 14:36) Ee Bwana, tunakuomba usitutie katika majaribu, bali utujalie nguvu ya kuvishinda vishawishi vyote. Tunawaombea wadhaifu, wagonjwa na wanaoteseka, ili uwape nguvu ya kufanya mapenzi yako. 2. Yesu Anapigwa Mijeledi Pilato akawaambia, "kwani ni ubaya gani alioutenda?" Wakazidi sana kupiga kelele, "Msulubishe!" Pilato akipenda kuwaridhisha makutano, akawafungulia Baraba; akamtoa Yesu, baada ya kumpiga mijeledi, ili asulubiwe. (Marko 15:14-15) Ee Bwana, wakati tunapokosewa haki, tunapodharauliwa na kutendewa ubaya bila sababu, tusaidie kuyakumbuka mateso yako. Tunawaombea haki wote wanaonyanyaswa, waliofungwa na wanaoteswa kwa ajili ya imani zao za kidini, kijamii na kisiasa. 3. Yesu Anavikwa Taji la Miiba Nao askari wakamchukua ndani ya behewa, ndio Praitorio (yaani nyumba ya uliwali), wakakusan...