Sala ya Huruma ya Mungu
ROSARI YA HURUMA YA MUNGU Baba yetu uliye Mbinguni..... Salamu Maria...... Nasadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi, muumba mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu Mwanae wa pekee Bwana wetu, aliyetungwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu; siku ya tatu akafufuka katika wafu, akapaa Mbinguni, amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi; kutoka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki, ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili, na uzima wa milele. Amina. Punje kubwa Baba wa milele, ninakutolea mwili na damu, Roho na Umungu, wa mwanao mpenzi sana Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima. Punje ndogo Kwa ajili ya mateso makali ya Bwana wetu Yesu Kristu; utuhurumie sisi na dunia nzima. X10 Kumalizia Mungu Mtakatifu, Mtakatifu mwenye enzi, Mtakatifu unayeishi milele, utuhurumie sisi na du...