Sala ya Huruma ya Mungu
ROSARI YA HURUMA YA MUNGU
Baba yetu uliye Mbinguni..... Salamu Maria......
Nasadiki kwa Mungu Baba Mwenyezi, muumba mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu Mwanae wa pekee Bwana wetu, aliyetungwa kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu; siku ya tatu akafufuka katika wafu, akapaa Mbinguni, amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi; kutoka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki, ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili, na uzima wa milele. Amina.
Punje kubwa
Baba wa milele, ninakutolea mwili na damu, Roho na Umungu, wa mwanao mpenzi sana Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zetu, na dhambi za dunia nzima.
Punje ndogo
Kwa ajili ya mateso makali ya Bwana wetu Yesu Kristu; utuhurumie sisi na dunia nzima. X10
Kumalizia
Mungu Mtakatifu, Mtakatifu mwenye enzi, Mtakatifu unayeishi milele, utuhurumie sisi na dunia nzima. X3
Ewe damu na maji, iliyomwagika kutoka moyoni mwa Yesu, kama chemichemi ya huruma kwetu, Tunakutumainia. X3
LITANIA YA HURUMA YA MUNGU
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie, Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
Kristo utusikie, Kristo utusikilize
Baba wa Mbinguni Mungu, Utuhurumie
Mwana, Mkombozi wa dunia, Mungu, Utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu mmoja, Utuhurumie
Huruma ya Mungu, iliyo sifa kuu ya Muumba wetu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo kilele cha ukamilifu kwa Mwokozi wetu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo upendo usiopimika wa Roho Mtakasa, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo fumbo lisilofahamika la Utatu Mtakatifu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo ishara ya uwezo mkuu wa Mungu Mwenyezi, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyofumbuliwa katika kuziumba Roho za Malaika wa Mbinguni, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyotuumba na kutuamuru tuwepo bila kutokana na chochote, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayoshika na kuushikiza ulimwengu mzima, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayotujalia maisha ya kutokufa, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayotukinga na adhabu tunazostahili, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayotuinua tutoke katika taabu, unyonge na maumivu ya dhambi zetu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayotufanya wenye haki katika Neno aliyejifanya mtu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayofurika kutoka katika Majeraha Matakatifu ya Kristo, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayobubujika toka ndani ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyotupatia Bikira Maria Mtukufu kabisa awe kwetu "Mama wa Huruma" , Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayoonyeshwa katika Ufunuo wa Mafumbo Matakatifu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyoonyeshwa katika kuanzishwa Kanisa Katoliki, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayopatikana katika mafumbo ya Sakramenti Takatifu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayotolewa kwa wanadamu wote kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo na Kitubio, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayotolewa kwa Sakramenti ya Ekaristi na Upadirisho, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayoonyeshwa kwetu pale inapotuita na kutuingiza katika imani Takatifu ya Kikristo, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayotimilika katika ukamilifu wa watu watakatifu, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, chemichemi ya afya kwa wagonjwa na wote wanaoteseka, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo faraja ya wote wenye uchungu moyoni, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo tumaini la roho zinazosumbuliwa kwa mkato wa tamaa, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo mwenzi wa daima na popote pa watu wote, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, inayowahi kutuletea neema zake, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo amani yao wanaokufa, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo burudisho na faraja yao marehemu Toharani, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo furaha ya Mbinguni kwa Watakatifu wote, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, iliyo Taji la Watakatifu wote, Tunakutumainia
Huruma ya Mungu, chemichemi ya miujiza isiyokauka, Tunakutumainia
Mwanakondoo wa Mungu uliyetuonyesha huruma yako kuu katika kuikomboa dunia kwa Msalaba wako Mtakatifu, Utusamehe Ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu unayejitolea kwetu kwa mapendo na huruma katika kila adhimisho la Sadaka ya Misa Takatifu... Utusikilize Ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu unayeondoa dhambi za ulimwengu kwa njia ya huruma yako isiyo na mwisho, Utuhurumie
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie, Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
K: Huruma anana za Bwana zi juu ya kazi zake zote
W: Huruma za Bwana nitaziimba milele
Tuombe:
W: Ee Mungu, uliye na huruma isiyo na mwisho, hazina za wema wako na upendo wako hazina mipaka. Tunakusihi ututazame sisi watu wako huku duniani, na kutuongezea huruma yako tena na tena, ili itusaidie tusije tukakata tamaa hata mara moja, haidhuru, hata tukikumbana na majaribu makubwa kiasi gani, bali tuweze daima kuzielekea, na kuzishika amri zako kwa matumaini, na kutimiza mapenzi yako matakatifu, ambayo ndiyo "Huruma yenyewe".
Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, Mwanao Mfalme wa amani na huruma, aishiye na kutawala nawe, na Roho Mtakatifu, kwa pamoja mkituonyesha huruma, daima na milele. Amina.
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie, Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
Kristo utusikie, Kristo utusikilize
Baba wa Mbinguni Mungu, Utuhurumie
Mwana, Mkombozi wa dunia, Mungu, Utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu mmoja, Utuhurumie
Huruma ya Mungu, iliyo sifa kuu ya Muumba wetu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo kilele cha ukamilifu kwa Mwokozi wetu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo upendo usiopimika wa Roho Mtakasa,p Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo fumbo lisilofahamika la Utatu Mtakatifu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo ishara ya uwezo mkuu wa Mungu Mwenyezi, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyofumbuliwa katika kuziumba Roho za Malaika wa Mbinguni, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyotuumba na kutuamuru tuwepo bila kutokana na chochote, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayoshika na kuushikiza ulimwengu mzima, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayotujalia maisha ya kutokufa, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayotukinga na adhabu tunazostahili, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayotuinua tutoke katika taabu, unyonge na maumivu ya dhambi zetu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayotufanya wenye haki katika Neno aliyejifanya mtu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayofurika kutoka katika Majeraha Matakatifu ya Kristo, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayobubujika toka ndani ya Moyo Mtakatifu wa Yesu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyotupatia Bikira Maria Mtukufu kabisa awe kwetu "Mama wa Huruma" , Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayoonyeshwa katika Ufunuo wa Mafumbo Matakatifu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyoonyeshwa katika kuanzishwa Kanisa Katoliki, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayopatikana katika mafumbo ya Sakramenti Takatifu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayotolewa kwa wanadamu wote kwa njia ya Sakramenti ya Ubatizo na Kitubio, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayotolewa kwa Sakramenti ya Ekaristi na Upadirisho, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayoonyeshwa kwetu pale inapotuita na kutuingiza katika Imani Takatifu ya Kikristo, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayotimilika katika ukamilifu wa watu watakatifu, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu chemichemi ya afya kwa wagonjwa na wote wanaoteseka, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo faraja ya wote wenye uchungu moyoni, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo tumaini la roho zinazosumbuliwa kwa mkato wa tamaa, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo mwenzi wa daima na popote pa watu wote Ninakutumainia
Huruma ya Mungu inayowahi kutuletea neema zake, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo amani yao wanaokufa, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo burudisho na faraja yao marehemu Toharani, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo furaha ya Mbinguni kwa Watakatifu wote, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu iliyo Taji la Watakatifu wote, Ninakutumainia
Huruma ya Mungu chemichemi ya miujiza isiyokauka, Ninakutumainia
Mwanakondoo wa Mungu uliyetuonyesha huruma yako kuu katika kuikomboa dunia kwa Msalaba Wako Mtakatifu, Utusamehe Ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu unayejitolea kwetu kwa mapendo na huruma katika kila adhimisho la Sadaka ya Misa Takatifu... Utusikilize Ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu unayeondoa dhambi za ulimwengu kwa njia ya huruma yako isiyo na mwisho, Utuhurumie
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie, Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie, Bwana utuhurumie
K: Huruma anana za Bwana zi juu ya kazi zake zote
W: Huruma za Bwana nitaziimba milele
Tuombe:
W: Ee Mungu uliye na huruma isiyo na mwisho, na hazina za wema na upendo wako hazina mipaka. Tunakusihi ututazame sisi watu wako huku duniani, na kutuongezea huruma yako tena na tena, ili itusaidie tusije tukakata tamaa hata mara moja, haidhuru, hata tukikumbana na majaribu makubwa kiasi gani, bali tuweze daima kuzielekea na kuzishika amri zako kwa matumaini, na kutimiza mapenzi yako matakatifu, ambayo ndiyo "Huruma yenyewe".
Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo, Mwanao Mfalme wa amani na huruma, aishiye na kutawala Nawe na Roho Mtakatifu, kwa pamoja mkituonyesha huruma daima na milele. Amina.